.
26th January, 2020
Wakaazi wa mji wa Garissa wamefanya maandamano ya amani kuishinikiza serikali kuimarisha usalama katika eneo hilo ili kuzuia mashambulizi ya mara kwa mara kutoka kundi la wanamgambo wa Alshabaab kutoka Somalia. Wakizungumza baada ya maandamano hayo, wanarakati kutoka kaunti ya gGarissa wakiongozwa na Mwalimu Salah Yusuf wamelaani shambulizi la hivi maajuzi lililowalenga wanafunzi pamoja na walimu.