.
25th January, 2020
Tunaanzia Mombasa katika bustani ya mama Ngina ambapo mkutano wa BBI ulifanyika na viongozi wa pwani kutoa maazimio yao kuhusu wanayotarajia katika mchakato wa BBI. Suala la ardhi lilipewa uzito mkubwa huku ardhi isiyojulikana wamiliki wake ikitakiwa kutwaliwa na serikali. Kiongozi wa ODM Raila Odinga na wenzake Kalonzo Musyoka wa wiper na Moses Wetangula walihudhuria hafla hiyo sawa na wabunge wanaoegemea mrengo wa naibu rais William Ruto wakiongozwa na seneta Kipchumba Murkomen