.
22nd January, 2020
Wakazi wa eneo la Weru, Kinangop kaunti ya Nyandarua wamepatwa na mshangao kufuatia kisa cha mwanamume mmoja mwenye umri wa umri 25 kudaiwa kumuua msichana mwenye umri wa miaka 22 kwa kumdunga kisu mara kadhaa katika kile kinachoonekana kuwa ni mzozo wa kimapenzi.Inadaiwa kabla ya mwanamme huyo kufanya kitendo hicho wawili hao walikuwa na mgogoro na kisha kutengana. Mwanamke aliyefariki alitambuliwa kwa jina la Consolata Wambui ambaye ni mwalimu katika shule ya upili ya St. Michael nae mshukiwa kwa jina Allan Musila alikuwa akifanya kazi ya ulinzi eneo la magharibi. Mshukiwa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Engineer.