.
22nd January, 2020
Abiria watatu wamejeruhiwa vibaya huku kumi na wanane wakipata majeraha madogomadogo baada ya basi walimokuwa wakisafiria kungongana ana kwa ana na lori yapata mita mia mbili kutoka kituo cha polisi cha juja kwenye barabara kuu ya Thika kaunti ya kiambu. Taarifa zinasema kuwa basi hilo la kampuni ya Neo kenya lenye uwezo wa kubeba abiria 52 lilikuwa likielekea mjini Thika kutoka nairobi alasiri ya leo wakati ajali hiyo ilipotokea na kusababisha msongamano mkubwa wa magari.