Kiu ya Elimu : Mwanafunzi awashangaza walimu baada ya kuripoti shuleni na kalamu 2 pekee
21st January, 2020
<style type="text/css">p.p1 {margin: 0.0px 0.0px 0.0px 0.0px; line-height: 20.1px; font: 15.0px 'Microsoft Sans Serif'}
span.Apple-tab-span {white-space:pre}
</style>
Mwanafunzi mmoja kutoka eneo la dandora kaunti ya Nairobi ameshangaza walimu katika shule ya upili ya igoki huko Imenti kusini baada ya kufika shuleni humo saa tatu usiku akiwa amejihami na kalamu mbili pekee. licha ya matatizo hayo Wycliffe Omondi alijitahidi kufika shuleni japo bila karo na walimu wakampokea. Katika kaunti ya Nakuru,msichana mmoja aliyekita kambi katika kituo cha polisi cha Central amepata afueni baada ya msamaria mwema kujitokeza kumlipia karo na mahitaji ya shuleni. Naomy Kwamboka sasa amejiunga na shule ya upili ya Morop.