20th January, 2020
<style type="text/css">p.p1 {margin: 0.0px 0.0px 0.0px 0.0px; line-height: 20.4px; font: 15.0px 'Microsoft Sans Serif'} span.Apple-tab-span {white-space:pre} </style>
Gavana wa West Pokot John Lonyangapuo amewaonya wahudumu wa afya wanaoonyesha uzembe kazini kwamba watapigwa kalamu. Lonyangapuo amesema hayo alipofika ghafla katika zahanati ya losam na kumpiga kalamu muuguzi mmoja aliyekosa kufika kazini bila sababu maalum. Alipowasili katika zahanati hiyo, ilikuwa saa moja asubuhi na kuipata milango imefungwa na muuguzi hayupo.