Mwana Blogu Nyakundi akamatwa kwa madai ya kutaka kuilaghai benki ya Victoria Sh17.5
20th January, 2020
<style type="text/css">p.p1 {margin: 0.0px 0.0px 0.0px 0.0px; line-height: 20.4px; font: 10.0px Arial}
span.s1 {font: 15.0px 'Microsoft Sans Serif'}
span.Apple-tab-span {white-space:pre}
</style>
Polisi wamemtia mbaroni mwanablogu Cyprian Nyakundi kwa madai ya kujaribu kuilaghai benki ya Victoria kiasi cha shilingi milioni 17.5. Polisi wanaarifu wakati wa kutiwa mbaroni kwa mwanablogu huyo alipatikana na shilingi zaidi ya milioni moja ambazo alikuwa tayari amelipwa na wasimamamizi wa benki hiyo ambao walikuwa wamemwekea
Mtego wakiwajumuisha polisi ili kumnasa. nyakundi aliripotiwa kuwa alikuwa amechapisha taarifa tatanishi kuhusu benki husika katika blogu, kisha baadaye akadai kulipwa pesa hizo ili kuifuta taarifa hiyo ambayo ingeiharibia sifa benki hiyo.wametiwa mbaroni akiwemo jamaa mwengine na sasa wanazuiliwa katika kituo cha polisi cha gigiri wakitarajiwa kufikishwa mahakamani hapo kesho.