18th January, 2020
Baadhi ya viongozi kutoka maeneo ya magahribi ambao walikuwa wamepanga kuandaa mkutano mjini Mumias leo walilazimika kukatiza mkutano huo baada ya polisi kushika doria katika uwanja huo wa bomani. Hata hivyo wale viongozi waliojaribu kuzungumza na wananchi kando kando ya barabara maeneo ya Mumias walifukuzwa kwa vitoa machozi. Na sasa, viongozi hao wameapa kuandaa mkutano wao wiki ijayo, huku wakidai kuwa mbunge wa Mumias mashariki Benjamin Washiali ametekwa nyara na mahasidi wake wa kisiasa.