.
18th January, 2020
Mkutano uliokuwa umesubiriwa wa BBI mjini Kakamega ulifanyika na kuhudhuriwa na kiongozi wa ODM Raila Odinga na viongozi wa magharibi Musalia Mudavadi, Moses Wetangula pamoja na katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli. Mbali na kupigia debe stakabadhi hiyo ya bbi baadhi walipendekeza kura ya maamuzi ifanywe haraka iwezekanavyo. Hata hivyo kulikuwa na maoni yalionekana kuwa kinzani kutoka kwa jinsi ya kusukuma ajenda ya BBI kutoka kwa kiongozi wa ANC Musalia Mudavadi.