×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Mwili wa mwanahabari Anjlee Gadhvi yateketezwa katika tanuri ya Kihindi Kariakor

11th January, 2020

Mwili wa mwanahabari wa runinga ya k 24 Anjlee Gadhvi umeteketezwa hii leo katika tanuri la kihindi iliyoko mtaa wa Kariokor jijini Nairobi.  Ibaada ya wafu ilifanyika katika ukumbi wa Lohana ulioko Forest Road, Mstakabala na Nairobi Gymkhana.
Marehemu Anjlee aliwahi kufanya kazi na shirika la KTN News kabla kujiunga na k 24.  Aliaga dunia siku ya ijumaa katika hospitali ya Aga Khan, Nairobi.  Jamaa na marafiki walijumuika kwenye ibaada ya wafu kutoa heshima zao za mwisho.  Marehemu Anjlee alikuwa akiuguza saratani ya mapavu na maini.  Aligunduliwa na saratani mwaka wa 2013 kufuatia uchunguzi kwa maabara.  Anjlee alifanyiwa matibabu humu nchini na nje ya nchi.  Mwaka 2018 alisafiri nchini india kupokea matibabu spesheli kwa jina ‘cyberknife procedure’ kwa minajili ya kupambana na kuangamiza saratani mwilini. Marehemu anjlee amemuacha mume na watoto wawili.

.
RELATED VIDEOS