.
7th January, 2020
Familia moja huko Bungoma inaitaka tume ya kuwajiri walimu, TSC, kumchukulia hatua mwalimu mmoja wa shule ya msingi, anayedaiwa kufanya mapenzi na binti yao kisha kumpiga picha akiwa uchi na kuzitundika picha hizo mitandaoni. Mwalimu huyo kutoka shule ya msingi ya Namutokholo, huko Sirisia kaunti ya Bungoma, anatuhumiwa kumpiga picha mwanafunzi wa kike wa kidato cha tatu akiwa uchi, na kisha kuzitundika picha za mwanafunzi huyo kwenye mtandao. Babake msichana huyo aliaga dunia hivi majuzi na inadaiwa kwamba mwalimu huyo aliahidi kwamba angemsaidia msichana huyo.