7th January, 2020
Mafuriko ambayo yamekuwa yakishuhudiwa katika sehemu mbali mbali za nchi sasa yameacha zaidi ya watu elfu kumi na tano waliokuwa wakiishi katika kambi mbali mbali bila makao. Maeneo yaliyoathrika pakubwa ni katika tanadelta ambako zaidi ya vijiji kumi vimefurika na kusababisha hasara kwenye mimea na nyumba.