31st December, 2019
Katibu mkuu wa muungano wa vyama vya wafanyakazi, COTU, Francis Atwoli, amewahimiza wanasiasa kuukaribisha mwaka mpya wa 2020 kwa kuvumiliana na kupeana heshima. Atwoli aliyezungumza nyumbani kwake huko Kajiado akiwa na familia yake, amewaonya wanasiasa dhidi ya kuzua maneno ya migawanyiko, akisisitiza kwamba mwaka mpya utakuwa wa ufanisi mkubwa ikiwa wakenya wataendelea kuheshimu yaliyomo kwenye ripoti ya BBI.