.
30th December, 2019
Wahudumu themanini na wawili wa bodaboda eneo la Kabati katika eneo bunge la Maragua kaunti ya Murang'a wameandikisha chama cha ushirika ambapo wananuia kujihusisha na biashara ya ujenzi wa nyumba kwa wanachama. Wahudumu hao hukutana kila Jumanne na kutoa michango ya shilingi mia tano kila mmoja kwenye hazina hiyo. Wanajivunia umoja wao ambao ulianza kwa kununua pikipiki nne na sasa wana malengo makuu.