.
18th December, 2019
Waziri wa elimu Profesa George Magoha ametangaza matokeo ya mtihani wa KCSE wa mwaka huu. Takriban wanafunzi laki saba waliufanya mtihani huo huku matokeo yakiashiria kuwa wasichana walifanya vyema kuliko wavulana huku wanafunzi waliopata chini ya alama mia mbili katika mtihani wa KCPE wakionyesha ukakamavu na kutoa matokeo bora. Waziri Magoha amesema wanafunzi elfu umoja mia tatu hawatapokea matokeo yao kutokana na udanganyifu.