16th December, 2019
Gavana wa Machakos Alfred Mutua hii leo aliandikisha taarifa ya polisi kwa madai kuwa maisha yake yapo hatarini. Mutua anadai kuwa Naibu wa Rais William Ruto, mbunge Adan Duale na Seneta Kipchumba Murkomen ni wakulaumiwa kwa vitisho hivo dhidi ya maisha yake. Akihutubia wanahabari katika kituo cha polisi cha Kilimani, Mutua sasa anataka usalama wake kudumishwa na wahusika kuchukuliwa hatua. Hata hivyo kupitia ukurasa wake wa twitter seneta Murkomen amemtaja Mutua kuwa mtu anayependa sarakasi hata wakati isipohitajika. Kadhalika Duale amejitenga na madai hayo