16th December, 2019
Mvulana mmoja mwenye umri wa miaka 14 aliyepashwa tohara anauguza majereha mabaya katika hospitali kuu ya Nakuru. Mvulana huyo anadai mlezi wake wa jandoni alimshambulia kwa chupa ya soda na kumjeruhi vibaya. Babake kijana huyo sasa analilia haki ya mwanawe kwani uchunguzi wa matibabu umebaini alijeruhiwa nyeti zake pia. Kisa hiki aidha kikiwa mojawapo wa vingi ambavyo vimesheni katika siku za hivi karibuni.