.
10th December, 2019
Viongozi wa siasa kutoka jamii ya wapokot wamemtaka Rais Uhuru Kenyatta atangaze mafuriko na maporomoko ya ardhi yanayosababishwa na mvua nyingi zinazozidi kunyesha kote nchini kuwa janga la taifa. Wakizungumza kwenye ibada ya wafu kwa watu walioangamia kwenye maporomoko ya ardhi yaliyosababishwa na mafuriko huko Pokot Magharibi, viongozi hao aidha wametoa wito kwa wanasiasa kusitisha mjadala kuhusu bbi hadi suluhu kwa majanga tofauti yanayolikumba taifa ipatikane.