10th December, 2019
Wiki moja baada ya mahakama kuu kusitisha utozaji wa ada mpya ya uegeshaji magari jijini nairobi, masaibu ya wenye magari hayajakoma huku washika dau husika wakilimbikiziana lawama ya nani wa kulaumiwa. Ada mpya ya shilingi 400 imeendelea kutozwa siku tatu baada ya uamuzi wa korti iliyoagiza kusitishwa kwake. Shirikisho la watumiaji bidhaa na huduma nchini cofek linadai kupeleka stakabadhi rasmi za agizo la mahakama kwa wakili mkuu wa kaunti alhamisi iliyopita jambo ambalo linatofautiana na taarifa ya serikali ya kaunti ya nairobi inayodai kupata stakabadhi hizo jana alasiri.