.
2nd December, 2019
Jumuiya ya Afrika Mashariki inatimiza miaka 20 tangu kuundwa upya baada ya jumuiya ya mwanzo kusambaratika mwaka 1977. Hata hivyo tathmini ya miaka 20 inaonesha kuwa jumuiya hiyo bado ina safari ndefu ya kutimiza lengo la kuanzishwa kwake. Maadhimisho ya sherehe hiyo ya miaka 20 yamefanyika katika makao makuu ya jumuiya hiyo mjini arusha nchini Tanzania. Mwanahabari wetu Rajabu Hassan yupo mjini Arusha na ifuatayo ni taarifa yake.