.
2nd December, 2019
Majina ya wanafunzi wa kujiunga na nafasi za kidato cha kwanza katika shule za kitaifa na zile za kaunti, yameshawekwa wazi. Shughuli hiyo imekamilika leo katika taasisi ya kukuza na kuunda mitaala nchini, KICD, ambapo waziri wa elimu Prof. George Magoha ameongoza shughuli hiyo. Magoha amesema kuwa hakuna mtahiniwa yeyote ambaye atazuiliwa kujiunga na kidato cha kwanza kutokana na kutomaliza kulipa karo.