.
6th November, 2019
Akina Mama wanaofanya biashara kote nchini wameshauriwa kujitokeza na kujiunga katika makundi ili kupata mikopo kutoka kwa serikali. Akizungumuza na wanahabariki mwenyekiti wa muungano wa wanawake katika biashara Mary Muthoni ameiomba serikali kubuni mbinu na mikakati ya kuwaweka wanawake katika nafasi bora ya kujitegemea na kuwa sehemu ya kuinua uchumi wa taifa hili. Muthoni aliteuliwa juzi kuwa mshindi wa tuzo ya mwanamke bora kwenye ulingo wa biashara ukanda wa Afrika mashariki.