5th November, 2019
Viongozi wa siasa kutoka kaunti ya Tharaka Nithi wametishia kwenda mahakama kuu kupinga matokeo ya idadi ya watu katika kaunti hiyo. Gavana Muthomi Njuki amesema matokeo yaliyoorodhesha kaunti hiyo kuwa na idadi ya watu laki tatu, tisini na tatu elfu, mia moja sabini na moja,haidhihirishi hali halisi. wanasiasa hao sasa wanataka shughuli ya kuhesabu watu irudiwe katika kaunti hiyo.