5th November, 2019
Watu kumi na mmoja wamekamatwa leo katika kaunti ya kisii kwa tuhuma za kujifanya watahiniwa wa mtihani unaoendelea wa KCSE. Maafisa wa elimu kwa ushirikiano na walinda usalama waliivamia shule ya binafsi ya Milimani Ramasha na kuwanasa washukiwa hao.