6th April, 2019
Kiongozi wa wengi katika bunge la taifa Aden Duale amesema kuwa sheria ya usawazishaji wa uwakilishi wa jinisia katika nafasi ya umma ni tatizo la kisiasa wala mahakama haitatoa suluhisho. Katiba ya Kenya ya mwaka 2010 inaelekeza ugavi wa nyadhifa za kuchaguliwa na uteuzi zisipite thuluthi mbili kwa jinsia moja. Mswada huo umeangushwa maara kadhaa bungeni.