2nd April, 2019
Gavana wa Kaunti ya Samburu Moses Lenolkulal ameachiliwa kwa dhamana ya shilingi milioni mia moja hasmini na mdhamini wa kiasi sawa na hicho au pesa taslimi shilingi milioni mia moja. Gavana huyo anaandamwa na kesi ya ufisadi ya kupokea mamilioni ya pesa kwa ajili ya utoaji wa huduma kwa kaunti yake kupitia kampuni yake.