.
27th March, 2019
Masuala ya ufisadi na haki kwa jamii zilitawala mazungumzo katika mkutano kati ya wahariri wa vyombo vya habari, mkurugenzi mkuu wa mashtaka ya umma noordin hajji na wadau mbalimbali katika sekta hiyo. Hajji ametoa wito kwa vyombo vya habari kutoa taarifa zaidi kuhusu sakata za ufisadi au ukosefu wa haki ili kusaidia katika ujenzi wa taifa. Alitoa hakikisho la kupunguza msongamano wa kesi haswa zinazohusiana na ufisadi ambazo zimeathiri uchumi wa taifa. Kwa upande wao waandishi wa habari wametilia mkazo kuwepo kwa vyombo huru vya habari na kutonyanyaswa kwa waandishi wanaotoa taarifa za sakata mbalimbali.