26th March, 2019
Mama Alice Shiundu amekuwa akiuza samaki katika mpaka wa Kenya na Uganda katika kituo cha mpakani cha malaba kwa miaka kumi sasa. Biashara yake humlazimu kuraukia nchini uganda anakowanunua samaki na kuja kuwauza nchini kenya na katika miji mingine. Sasa amekuwa maarufu sana wanunuzi wake wakitoka maeneo mbali mbali.