25th March, 2019
Kuna baadhi ya watu katika jamii wanaochukulia ulemavu kama kizuizi cha kuafikia ndoto zao ilhali wengine huchukulia hali hiyo kama fursa ya kujiendeleza. Mmoja wa watu watu hao ambao wamechukulia ulemavu kama fursa ni Lokuta Ewoi ambaye amekuwa katika msitari wa mbele kupigania haki za watu wenye ulemavu na kuondoa dhana kuwa watu kama yeye hawana uwezo wa kufanya kazi kama watu wengine.