×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Mshukiwa wa madawa ya kulevya afikishwa mahakamani

25th March, 2019

Mfanyabiashara mmoja maarufu jijini mombasa amefikishwa mahakamani baada ya kukamatwa siku ya jumamosi akiwa na kilo moja ya dawa aina ya heroin yenye thamani ya shilingi milioni 1.5. Abdul majid msallam timami aliye na umri wa miaka 47 amefikishwa katika mahakama ya mombasa leo ambapo amesomewa mashtaka dhidi yake. 

Kulingana na idara ya upelelezi, dci dawa hizo zilikuwa zimefichwa ndani ya mfuko na zilikuwa zikisafirishwa kwa gari aina ya honda.timami anashtumiwa kuwatumia vijana kuziuza dawa hizo, hali ambayo imesababisha wengi wao kukosa kwenda shuleni na badala yake kujiingiza katika biashara haramu ya ulanguzi wa dawa za kulevya.aidha ameshtumiwa kumiliki malori makubwa makubwa katika ukanda wa afrika mashariki huku akiyatumia katika biashara haramu.inaarifiwa amekuwa akiendesha biashara hiyo kwa kipindi cha mwongo mmoja katika eneo la tudor kaunti ya mombasa.mahakama imemwachilia kwa dhamana ya shilingi millioni moja.kesi hiyo itaskizwa aprili 14.

.
RELATED VIDEOS