.
19th March, 2019
Seneta wa Baringo Gideon Moi ameongoza shughuli ya kugawa chakula cha msaada kwa waathiriwa wa baa la njaa huko baringo. Takriban watu elfu sabini na tatu katika kaunti ya baringo wanakabiliwa na baa la njaa. Kutokana na hilo hii leo chakula cha msaada kimeanza kutolewa kwa wenyeji. Kaunti ya baringo ni miongoni mwa kaunti 12 ambazo zimeathiriwa na baa la njaa.