19th March, 2019
Alasiri ya leo kimeripotiwa kisa cha kupatikana kwa sarafu za kigeni katika benki ya barclays tawi la queensway. Sarafu hizo ilivyoarifiwa na benki hiyo kwenye mtandao wake wa twitter, zinadaiwa zilikuwa kwenye kisanduku maalum cha mteja mmoja, aliyezuiliwa na maafisa wa flying squad baada ya kubainika kwamba kisanduku hicho anachoruhusiwa kukitumia kuhifadhi fedha zake, awali kiliripotiwa kuwa na sarafu bandia za dollar za marekani za jumla ya shilingi bilioni kumi na saba kabla ya maafisa wa dci kudai baadaye kuwa hela hizo zilikuwa kima cha shilingi billioni mbili. Benki hiyo imeahidi kushirikiana na polisi kwenye uchunguzi huo, kisa ambacho kimeibua hisia mseto kwenye mitandao ya kijamii.