.
19th March, 2019
Mbunge wa zamani wa Mbooni Kisoi Munyao amelaumiwa kwa kuwalaghai wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali ya nchi kwa kuwaahidi ufadhili wa masomo kupitia Shirika lake lisilokuwa la serikali la The Kenya Youth Education fund kwa ushirikiano na chuo cha Foundation Institute of Africa. Inadaiwa Wanafunzi mia tatu hamsini walipokea ufadhili huo wa kusoma huku wakitakiwa kulipa takriban shilingi elfu ishirini ili kusajiliwa, na sasa wanafunzi hao hawako darasani wala nyumbani kwao.