.
12th March, 2019
Hakimu anayehusishwa na mauaji ya mumewe ambaye alikua wakili pamoja na washukiwa wengine 3 wametakiwa kupimwa akili. Wanne hao walifikishwa kizimbani katika mahakama ya machakos, huku mahakama ikiamuru ripoti ya hali ya akili zao kabla ya kuanza kusikizwa kwa kesi yao. Wakifika mbele ya naibu wa msajili mkuu Kipchumba Kenei, aliamua kuendelea kuwazuia pauline chesang katika kituo cha athi river, huku sajenti richard moru, lawrence lempesi ambaye ni afisa wa nis aliyestaafu na constebo maundu mbithi kuzuiwa katika gereza la Machakos. Wataendelea kuzuiliwa hadi aprili 9 ambapo watahitajika kufika tena mahakamani.