.
4th March, 2019
Kiongozi wa huduma ya repentance and holiness prophet David Owuor amewekwa katika darubini hii leo familia ya mmoja wa wachungaji wake ikidai kuwa ni mlaghai. Familia ya mchungaji Jane Njagi inadai kuwa owuor kwa zaidi ya mwongo mmoja amekuwa akitumia mali ya mama huyo kuendesha huduma zake huku wakimnyima fursa ya kutangamana na familia yake pamoja na kumilki stakabadhi zake.