.
19th February, 2019
Sarakasi ilizuka katika Bunge la Kaunti ya Kisumu alasiri ya leo pale waakilishi wadi walitofautiana juu ya uamuzi wa kumuondoa mwenyekiti wa kamati ya bajeti stephen owiti. Walibadilishana makonde baada ya mwafaka kukosekana, kundi moja likiafiki kuapishwa kwa mwenyekiti mpya wa kamati hiyo, judith ogada. Taharuki ilianza wakati kiongozi wa wengi bungeni humo kenneth onyango alipouliza njia zilizotumiwa kumuondoa owiti kwenye wadhifa huo. Spika onyango oloo alikuwa akisimamia shughuli za kikao cha bunge hilo.