18th February, 2019
Mahakama imewaagiza viongozi wanne wa muungano wa wauguzi wakiwemo katibu mkuu seth panyako,naibu wake maurice opetu, msaidizi wao asha ali ido na mwenyekiti w akitaifa john gwasi kufika mbele ya mahakama hiyo siku ya jumanne tarehe 26 mwezi huu, kujibu mashtaka ya kupuuzilia mbali agizo la korti, lilowataka kuuzima mgomo wao. Kauli zilizowasilishwa na baraza la magava kupitia wakili wao eugene lawi, ni kuwa wauguzi walipokezwa amri ya mahakama ikiwataka kutupilia mbali mgomo kwa ajili ya mazungumzo, ila wakili ya wauguzi alishikilia kuwa bado wauguzi hawajapokezwa amri hiyo. Hata hivyo jaji nelson abuodha aliyeskiza kesi hiyo alisema kuwa wauguzi walikuwa na maarifa kuhusu amri hiyo na matamashi yoyote katika vyombo vya habari ikiungaa mkono mgomo huo utatazamwa na mahakama hiyo kama ukaidi wa sheria za mahakama.