.
18th February, 2019
Viongozi wa siasa wametoa maoni mbalimbali kuhusu mzozo uliopo wa umiliki wa sehemu ya bahari hindi kati ya mpaka wa kenya na somalia. Waziri wa zamani wa mambo ya nje moses wetangula, mbunge wa aldas adan keynan na naibu spika wa senate prof. Kindiki kiture wamesema suala hilo linatakiwa kushughulikiwa kwa tahadhari. Kenya ilimwagiza balozi wake somalia lucas tumbo kurejea kwa mashauriano zaidi sawa na kumtaka balozi wa somalia kenya kuondoka.