16th February, 2019
Shule ya msingi ya moi kabarak huko nakuru hii leo imeandaa sherehe za shukrani kufuatia matokeo mazuri katika mitihani ya kitaifa kcpe mwaka uliopita. Kulingana na mwalimu mkuu wa shule hiyo nelson kiptoo, siri yao ya mafanikio imetokana na hofu ya mungu, bidii, umoja na kujitolea kwa wadau husika.