.
16th February, 2019
Polisi katika Kaunti ya Kakamega wameanzisha uchunguzi kutokana na mauti ya mwanafunzi mmoja. Mwanafunzi huyo wa kidato cha tatu katika shule ya wasichana ya butere alipatikana kwenye bweni akiwa amefariki. Inakisiwa kuwa msichana huyo aliyetambuliwa kama elizabeth musoi alipotea wakati wa mapumziko ya adhuhuri kabla ya maiti yake kupatikana. Bado haijabainika kama alijitia kitanzi au aliuwawa.