×
× KTN KTN News KTN Morning Express KTN Leo Leo Mashinani The Big Story Checkpoint News Center E-Paper Lifestyle & Entertainment Nairobian Entertainment Eve Woman Travelog TV Stations KTN Home KTN News KTN Farmers TV Radio Stations Radio Maisha Spice FM Vybez Radio Enterprise VAS E-Learning Digger Classified Jobs Games Crosswords Sudoku The Standard Group Corporate Contact Us Rate Card Vacancies DCX O.M Portal Corporate Email RMS
Login
×
Show Swahili

Wakulima nchini watalazimika kusubiri zaidi kupokea mbolea ya bei nafuu

11th February, 2019

Wakulima nchini watalazimika kusubiri zaidi kupokea mbolea ya bei nafuu kutoka kwa serikali, huku wizara ya kilimo kupitia halmashauri ya nafaka nchini ncpb ikiwa bado haijawajibikia matumizi ya takriban shilingi bilioni 2.1. Waziri wa kilimo mwangi kiunjuri ameeleza kamati ya bunge kuwa japo uchunguzi bado haujakamilika, wizara hiyo inaweza aidha kuagiza mbolea kupitia mfumo wa ununuzi ulioidhinishwa chini ya kipengee 114 cha sheria kuhusu ununuzi wa bidhaa, au kupitia makampuni ya binafsi. Hata hivyo, amefafanua kuwa endapo utaratibu utakaokubalika ni ununuzi kwa mujibu wa kipengee 114, wakulima bado watasubiri siku 21 kabla ya kupokea mbolea. Kwa mujibu wa kamati ya bunge, taifa linakodolea macho hatari ya uhaba wa chakula endapo suluhu ya haraka haitapatikana, kwa kuwa msimu wa upanzi unatarajiwa kuanza kufikia mwishoni mwa mwezi huu.

.
RELATED VIDEOS