.
11th February, 2019
Wafanyakazi wa Kaunti ya Nairobi wametangaza kuandaa mgomo na kuvuruga shughuli zote jijini kuanzia hapo kesho ili kushinikiza utekelezaji kikamilifu wa makubaliano ya mkataba. Katibu mkuu wa muungano wa wafanyikazi wa serikali za kaunti nchini, roba duba, amesema mgomo huo umetokana na hatua ya wizara ya fedha kukataa kutoa fedha kwa serikali ya kaunti ya nairobi kwa ajili ya kuwalipa wafanyikazi kwa mujibu wa makubaliano hayo ambayo sasa yamesajiliwa katika mahakama ya kutatua mizozo ya uajiri.