.
2nd February, 2019
Hatimaye, Mwendazake James Oduor Radido, alaarufu Cobra, alizikwa kwao Ukwala, katika eneo bunge la Ugenya. Mamia ya jamaa na marafiki walifika kumuaga Oduor, ambaye aliuawa katika shambulizi la kigaidi katika hoteli ya Dusit D2 katika eneo la westlands janauari kumi na tano. Marafiki na wengi wa waliomtambua akiwa hai walisema kuwa alikuwa mtu mwenye furaha na mwenye kutangamana na watu kwa urahisi. Oduor ambaye alikuwa mchezaji wa soka, amemwacha mjane diana otieno, na watoto wao wawili Janelle Akinyi, na Giovani Ochieng.