.
27th January, 2019
Maafisa wa polisi wanawahoji watu wanne wa familia moja kutoka eneo la Mbungoni kaunti ya Kilifi kwa madai ya mauaji.
Hii ni baada ya mwili wa kasisi Cosmas Hanjari wa Kanisa la Kimethodisti kupatikana ukining’inia kwenye chuma cha dirisha nyumbani kwake katika kile kinaonekana kuwa ni kisa cha kujitia kitanzi.
Miongoni mwa wale wanaozuiliwa na polisi ni mjane wa marehemu pamoja na wanawe wawili wa kiume.