22nd January, 2019
Uongozi wa chama cha KANU umesema kwamba utaendelea kupeana ushirikiano wake katika salamu za heri kati ya rais uhuru kenyatta na kiongozi wa ODM Raila Odinga. Akizungumza sehemu ya kipkok huko sigowet kaunti ya kericho, viongozi hao wakiongozwa na mwenyekiti wake gideon moi na mbunge wa tiaty william kamke, wamesema kwamba hatua zilizochukuliwa na rais kenyatta na raila odinga, zafaa kuungwa mkono na kwamba sio wakati wa kujadili siasa za mwaka. Wamewataka wanaoendelea na siasa, waache kufanya hivyo na kushughulikia swala la maendeleo ya taifa.