.
7th January, 2019
Viongozi wameombwa kukoma siasa na badala yake kulenga kutimiza ahadi za wakati wa kampeni kwa wananchi. Akizungumza katika kanisa la AIC Cheribo huko Kericho, naibu askofu mkuu wa kanisa la AIC katika eneo hilo la South Rift Johnstone Cheruiyot amesema ni mapema sana kwa viongozi kuanza mjadala wa siasa za urithi wa mwaka 2022.Hata hivyo Cheruiyot ameipongeza serikali kwa kuhakikisha kuwa kila mwanafunzi anapata elimu ya sekondari.