5th January, 2019
Mabingwa watetezi Gor Mahia wanatarajiwa kukosa huduma za wachezaji wao muhimu Harun Shakava, Francis Mustafa, Boniface Oluoch, Joash Onyango na Kenneth Muguna katika mechi ya ligi kuu ya taifa dhidi ya Mathare United siku ya jumapili. Lakini licha ya kukosa huduma za wachezaji hao , mkufunzi wa Gor Mahia Hassan Oktay ana imani kwamba wataandikisha matokeo mema dhidi ya Mathare. Kogalo wanashikilia nafasi ya tisa katika jedwali la ligi kuu nchini na alama sita.