5th January, 2019
Viongozi kutoka eneo la Magharibi sasa wameapa kuwa watawaadhibu vikali wanasiasa kutoka eneo hilo ambao wameonyesha dalili kuunga mkono azma ya Naibu wa Rais William Ruto kugombea kiti cha urais katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2022. Wamesisitiza kuwa anayepaswa kuungwa mkono kutoka eneo hilo ni kiongozi wa chama cha ANC Musalia Mudavadi.