.
3rd January, 2019
Watu sita wanaoaminika kuwa wa familia moja wamefariki papo hapo baada ya gari aina ya saloon walilokuwa wakisafiria kugongana ana kwa ana na lori kwenye barabara ya kericho? nakuru. Miongoni mwa majeruhi wa ajali hiyo ya mwendo wa saa saba kasorobo mchana wa leo ni watoto watatu na wavulana wawili waliokuwa wakirejea shuleni. Baadhi ya walioshuhudia ajali hiyo hata hivyo wanasema gari hilo aina ya saloon lilikuwa likiendeshwa kwa mwendo wa kasi. Miili ya waliofariki ilipelekwa katika hifadhi ya maiti ya hospitali ya kericho.