.
19th December, 2018
Mpango wa rais Uhuru Kenyatta wa kugharamia makazi nafuu kwa wakenya hatimaye umepata pigo ghaya baada ya mahakama inayoshughulikia maswala ya wafanyikazi kusitisha kwa muda kutekelezwa kwa mpango huo. Katika kesi iliyowasilishwa na muungano wa vyama vya wafanyikazi nchini COTU uamuzi umetolewa na jaji Hellen Wasilwa kusitisha kwa utekelezai kutoza asilimia 1.5 ya mishahara ya wafanyakazi wa serikali.